
Lowassa amesema kuwa halijui shamba alilolizungumzia Waziri huyo na kwamba hakuna ardhi ambayo anaimiliki kinyume cha taratibu.
Alisema
kuwa hana taarifa kamili kuhusu maelezo ya Waziri Lukuvi na kwamba
ameomba Mbunge wa Jimbo la Monduli, Julius Kalanga (Chadema)
kulifuatilia kwa karibu na kumpa taarifa ili aweze kulitolea ufafanuzi.
“Nashindwa
kutoa maelezo kuhusu taarifa hizo kwa sababu sifahamu lolote kuhusu
shamba hilo,” Lowassa anakaririwa na gazeti la Jambo Leo lililofanya nae
mahojiano kwa njia ya simu.
“Mimi
sipo Bungeni, nimesikia hizo habari, lakini sijui zimetolewa lini na
nani. Mbunge wangu analifanyia kazi kwa sababu sina shamba
nilalolimiliki ambalo liko kinyume na taratibu,” aliongeza.
0 comments:
Post a Comment