Friday, 27 May 2016

Diamond achukua taji la Lip Sync Africa ya MTV

Diamond Platnumz amechukua taji la kipindi cha Lip Sync Africa kinachorushwa na kituo cha MTV SA.
13248947_844312172340600_275142530_n
13248947_844312172340600_275142530_n
D’Banj ambaye ni host wa show hiyo akimpongeza Diamond kwa ushindi
Alikuwa akichuana na mshkaji wake, Theo wa kundi la Mafikizolo. Kwenye kipindi hicho, wasanii wawili hushindana kuziimba nyimbo za wasanii wengine kwa kugandamizia na kupatikana mshindi mmoja.
Baada ya kuchukua ushindi huo na kupewa mkanda wake, Diamond aliandika kwenye Instagram: Ningependa kumshukuru Mwenyezi Mungu na kuwajuza kuwa kijana wenu nimewawakilisha vyema kwenye mashindano ya LIP SYNC BATTLE AFRICA ya @MtvBaseAfrica na kuweza kuibuka kidedea kwenye Mashindano ya Stage hiyo na kunyakua Mkanda.”
13181345_179733292424560_2022858402_n
13181345_179733292424560_2022858402_n
Naye Theo alikubali kushindwa na kumpongeza Diamond kwa ushindi huo.
13267326_1112449035442570_1532958103_n
Lip Sync Battle ni show iliyoanzia Marekani na kuongozwa na rapper LL Cool J na mke wa John Legend, Chrissy Teigen. Kwa Afrika show hiyo inaongozwa na mrembo wa Afrika Kusini Pearl Thusi na staa wa Nigeria, D’Banj.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 

MAISHA TM Copyright © 2012 Template Designed by BTDesigner Published..Blogger Templates· Powered by Blogger